Mkutano Mkuu wa 21 wa KKKT

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa 21 wa KKKT wametakiwa kuhakikisha wanaepukana na masuala ya rushwa katika uchaguzi mkuu wa kumpata Mkuu wa Kanisa hilo unaotarajiwa kufanyika Alhamis ya Agosti 24 , 2023.Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania ambaye pia ni Mkuu wa Dayosisi ya Kaskazini Askofu Dkt Fredrick Onael Shoo, anayemaliza muda wake ametoa onyo hilo Jumanne Agosti 22, 2023 wakati akifungua Mkutano Mkuu wa 21 ambapo wajumbe wanatarajia kufanya uchaguzi wa kumchagua Mkuu wa KKKT.Dkt Shoo amewataka wajumbe hao kutofautisha uchaguzi huo wa mkuu wa Kanisa na chaguzi zinazofanyika sehemu nyingine kwani anae muweka kiongozi yeyote wa Kanisa kwenye mamlaka ni Mungu pekeeAmesema mjumbe yeyote atakae toa au kupokea Rushwa basi fedha hizo ziungue mifukoni mwao.