Askofu Dkt. Shoo amstaafisha Mch. Leonard Kessy Usharika wa Wiri

Askofu Dkt. Shoo amstaafisha Mch. Leonard Kessy Usharika wa Wiri

Ofisi yafunguliwa Lengongu

Tuitikie Wito kwa Moyo Mnyofu

Mkuu wa KKKT na Dayosisi ya Kaskazini Askofu Dkt. Fredrick Onael Shoo, ameongoza Ibada ya kumstaafisha kwa heshima Mch. Leonard Kessy, Ibada iliyofanyika katika Usharika wa Wiri mtaa wa Ebenezer Jimbo la Siha Oktoba 22, 2023.

Ibada hiyo ilitanguliwa na ufunguzi wa Ofisi ya Mtaa wa Lengongu iliyogharimu kiasi cha shilingi milioni 92, fedha zilizochangwa na washarika. Tendo hilo lilifanywa na Askofu Dkt. Fredrick Shoo akishirikiana na Msaidizi wa  Askofu Mch. Deogratius Msanya na Mkuu wa Jimbo la Siha Mch. Elisa Kileo.

Katika ibada hiyo Askofu Dkt. Shoo alimpongeza Mch. Kessy kwa kustaafu kwa heshima na kusema kuwa ni jambo la kumshukuru Mungu pale mtumishi anapomaliza wito wa utumishi wake salama. Pia alipongeza Usharika kwa maono mazuri ya ujenzi wa Ofisi ya Kisasa yenye ukumbi wa mikutano na chumba cha kulala cha watumishi wageni.

Mch. Leonard Kessy alianza huduma ya Uchungaji mwaka 1990 na alitumika katika sharika za Makivaru Meru mwaka 1990-1992, Naibili mwaka 1993-1998, Wiri mwaka 1999-2005, Olmolog 2006, Ngaritati na Wiri 2006-2009, Ivaeny  2010-2021 na Usharika wa Nasai Oktoba 2021-2022. Mchungaji ametumika kwa miaka 32.

Akihubiri katika ibada hiyo Msaidizi wa Askofu Mch. Deogratius Msanya aliwataka Watumishi na Wakristo kwa ujumla kutii wito kwa kugeuka na kuacha maovu. Alisema Mungu anatuita kutoka katika njia zisizofaa na kuwa wasafi ndipo tukatumikie wito aliotuitia.